Sunday, March 26, 2017

Gari la Uber linalojiendesha lasababisha ajali Marekani

Gari moja linalojiendesha kutoka kampuni ya Uber limepata ajali kwa kugongana na gari lingine huko nchini Marekani katika jimbo la Arizona,
Picha zimeonyesha gari hilo likiwa limepinduka lakini bado hakuna taarifa zozote za majeruhi.
Kituo kimoja cha televisheni kimeripoti kuwa dereva wa gari lililohusika katika ajali na gari la Uber hakuipisha gari hiyo.
Hatahivyo haijulikani iwapo gari hilo la Uber lilikuwa kwenye mfumo wa kuendeshwa bila dereva au la .
Huduma hiyo ya kampuni ya Uber ya magari yanayojiendesha bila dereva ilianza safari zake za uchukuzi mjini Arizona mwezi uliopita, ikiongeza uchukuzi wa safari hiyo kwenye miji mengine kama vile Pittsburgh na San Francisco

No comments:

Post a Comment

MASHINE ZA UMWAGILIAJI

 PATA MASHINE ZA UMWAGILIAJI KWA BEI NAFUU TUPO SOKO KUU LA KISUTU GOROFA YA TATU DUKA NO 44 CONTACT 0685476657