Jumla ya ombaomba sitini (60) wamekamatwa katika msako wa ombaomba unaoendelea katika jiji la Dar es Salaam.
Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Grace Magembe alipokuwa akitoa majibu ya uwepo wa ombaomba katika jiji la Dar es Salaam licha ya kuwepo kwa operesheni ya kuwaondoa.
Dk Magembe amesema bado ombaomba wamekuwa wakionekana jijini Dar es Salaam kutokana na kuwapo kwa watu wanaotoka mikoani na kuingia katika makundi ya ombaomba kila siku.
Amesema uongozi wa mkoa unashirikiana na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kutoa elimu mikoani kuhusu operesheni ya kuwaondoa ombaomba.
Amesema ombaomba wengi wanakuja kutoka maeneo mbalimbali ya nchi.
Awali Makonda alitangaza operesheni kubwa ya kuondoa ombaomba katika Jiji la Dar es Salaam.
aliwataka polisi kwa kushirikiana na ustawi wa jamii kuwaondoa ombaomba wote waliopo mitaani.
Pia, Makonda amepiga marufuku wananchi wanaowapa fedha ombaomba kuacha mara moja ili wajitafutie riziki wenyewe kwa kufanya biashara au kurudi mikoani kujishughulisha na kilimo.
No comments:
Post a Comment