Sunday, March 16, 2014

Arsenal yailaza Tottenham Spurs 1-0


Klabu ya Arsenal leo imeimarisha ari yake ya kutaka sana kushinda kombe la ligi kuu ya Premier kutokana na bao la pekee la Tomas Rosicky ambalo limeinua zaidi matumaini ya Gunners dhidi ya Tottenham.
Rosicky aliingiza bao lake dakika chache tu baada ya mchezo kung'oa nanga. 

Mchezaji wa Tottenham Emmanuel Adebayor alijaribu bahati ya kuingiza bao katika kipindi cha kwanza Tottenham ikiwa imedhibiti mchezo ingawa hakufua dafu.
Mkwaju wake Nacer Chadli ulizuiwa kwenye msitari wa lango huku mkwaju wake Adebayor ukiwa umepoteza mwelekeo sana lakini Arsenal hawakuishiwa matumaini.
Ushindi huu una maana kuwa Arsenal wanashikilia nafasi ya tatu katika jedwali la alama lakini wakiwa nyuma ya kiongozi Chelsea kwa alama nne.
Chelsea walishindwa bao moja Bila na Aston Villa katika mechi ya

No comments:

Post a Comment

MASHINE ZA UMWAGILIAJI

 PATA MASHINE ZA UMWAGILIAJI KWA BEI NAFUU TUPO SOKO KUU LA KISUTU GOROFA YA TATU DUKA NO 44 CONTACT 0685476657